Home » » TLTC yakarabati gari la zimamoto Moro

TLTC yakarabati gari la zimamoto Moro

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
KAMPUNI ya Tumbaku Tanzania (TLTC) imekarabati moja ya magari manne ya zimamoto mkoani Morogoro kwa gharama ya sh milioni 7.8 ili kusaidia idara hiyo kuboresha huduma zake.
Akikabidhi gari hilo lililokarabatiwa mjini Morogoro jana, Mkurugenzi wa Sheria na Uhusiano wa TLTC, Richard Sinamtwa, alisema kampuni iliamua kukarabati gari hilo  ikiwa ni kuunga mkono juhudi za serikali kujihami na majanga ya moto mkoani humo.
“Sisi kama moja ya jamii na raia wema wa Tanzania, tuliona kuwa kwa kukarabati gari hili tunaiunga mkono serikali kupitia ushirikiano wa serikali na taasisi binafsi katika uboreshaji wa huduma za zimamoto,” alisema.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa