Home » » 'MAJI HATARINI KUVUNJA NDOA ZA WATU MORO‘

'MAJI HATARINI KUVUNJA NDOA ZA WATU MORO‘

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Wanawake wa Mikese na Mkambarani mkoani Morogoro, wameiomba Serikali kuwatatulia kero sugu ya maji iliyodumu kwa muda mrefu kiasi cha kusababisha ndoa zao kuingia kwenye migogoro kutokana na kutumia muda mwingi kutafuta na kuziacha familia bila kuwa uangalizi wa kutosha.
Wakizungumza na gazeti hili katika Kijiji cha Fulwe Kata ya Mikese, mkoani Morogoro, Anna Massawe na Justina Eliasi walisema kero ya maji imekuwa kubwa na wanalazimika kutembea umbali wa kilometa 15 kila siku kusaka maji.
“Kweli ndoa zetu zipo hatarini kwa kuwa muda mwingi tunashinda kutafuta maji. Familia inakosa malezi ya karibu ya mama. Waume nao wanakuwa mbali nasi kwa muda mwingi,” alisema Anna massawe.
“Kila wakati wa uchaguzi unapofika, ahadi za viongozi ni kutatua kero ya kukosa maji, wakishaingia madarakani hakuna anayekumbuka. Maisha haya mpaka lini?” alihoji.
Akizungumzia hali hiyo, Diwani wa Kata ya Mwega, Jafari alisema Serikali imesikia kilio cha wakazi wa eneo hilo na kwamba iko kwenye mkakati wa kumaliza kero hiyo.
“Serikali inatambua adha na kero ya ukosefu wa maji kwenye kata hii, tayari tumeshaunda kamati maalumu ya kufuatilia tatizo hili. Nadhani muda siyo mrefu tutapata majibu,” alisema Jaffari. Wanawake wa Mikese na Mkambarani mkoani Morogoro, wameiomba Serikali kuwatatulia kero sugu ya maji iliyodumu kwa muda mrefu kiasi cha kusababisha ndoa zao kuingia kwenye migogoro kutokana na kutumia muda mwingi kutafuta na kuziacha familia bila kuwa uangalizi wa kutosha.
Wakizungumza na gazeti hili katika Kijiji cha Fulwe Kata ya Mikese, mkoani Morogoro, Anna Massawe na Justina Eliasi walisema kero ya maji imekuwa kubwa na wanalazimika kutembea umbali wa kilometa 15 kila siku kusaka maji.
“Kweli ndoa zetu zipo hatarini kwa kuwa muda mwingi tunashinda kutafuta maji. Familia inakosa malezi ya karibu ya mama. Waume nao wanakuwa mbali nasi kwa muda mwingi,” alisema Anna massawe.
“Kila wakati wa uchaguzi unapofika, ahadi za viongozi ni kutatua kero ya kukosa maji, wakishaingia madarakani hakuna anayekumbuka. Maisha haya mpaka lini?” alihoji.
Akizungumzia hali hiyo, Diwani wa Kata ya Mwega, Jafari alisema Serikali imesikia kilio cha wakazi wa eneo hilo na kwamba iko kwenye mkakati wa kumaliza kero hiyo.
“Serikali inatambua adha na kero ya ukosefu wa maji kwenye kata hii, tayari tumeshaunda kamati maalumu ya kufuatilia tatizo hili. Nadhani muda siyo mrefu tutapata majibu,” alisema Jaffari.
 Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa