Home » » Polisi yatoa onyo kwa wafanyabiashara Moro

Polisi yatoa onyo kwa wafanyabiashara Moro

Jeshi la Polisi mkoani Morogoro limewataka wafanyabiashara wenye mashine za EFD wanaolazimishwa kufunga maduka yao na kikundi cha wafanyabiashara wachache wasio na mashine hizo kutoa taarifa ili sheria ifuate mkondo wake.
Kauli hiyo imetolewa jana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Faustin Shilogile, kufuatia baadhi ya wafanyabiashara kulalamika kuwa kuna kundi la wahuni linalotumiwa na baadhi ya wafanyabiashara kuwashinikiza wengine kufanya mgomo ili kupinga mashine hizo.
Alisema mfanyabiashara akifunga duka lake kwa matakwa yake mwenyewe si kosa, lakini asilazimishe wengine kufunga maduka, kwani kufanya hivyo ni kutenda kosa.
"Jeshi la Polisi linafanya doria katika kila mtaa ili kukichunguza kikundi hicho kinachozuia wafanyabiashara wengine kufungua maduka," alisema Shilogile.
Alisema kuwa Jeshi la Polisi lipo kwa ajili ya ulinzi wa raia na mali zao ikiwa pamoja na kusimamia sheria za nchi zilizowekwa kwa mujibu wa katiba ya nchi, hivyo hakuna sababu ya kunyamazia matukio yeyote yenye nia ya kuvunja sheria zilizotungwa kwa mujibu wa sheria ya nchi," alisema.
Jana wafanyabiashara wa manispaa ya Morogoro walifunga maeneo yao ya biashara zao kwa lengo la kugomea matumizi ya mashine za kielektroniki za EFD

Chanzo;Majira

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa