Home » » Moro yaondoa mabango yasiyolipa kodi

Moro yaondoa mabango yasiyolipa kodi

MANISPAA ya Morogoro imeanza zoezi la kuvunja na kuondoa mabango ya biashara ambayo hayalipi kodi kwa manispaa hiyo, ambapo zaidi ya sh milioni 370 zinadaiwa kutoka kwa wamiliki wa mabango  hayo.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, Ofisa Uhusiano wa manispaa hiyo, Lilian Henerico, alisema manispaa imeamua kuondoa mabango hayo ili wahusika wanaodaiwa kulipa, ikiwa ni pamoja na kulipa faini kutokana na kuchelewa kulipa.
Alisema zoezi hilo ni la siku  14 na wameanza na mabango ya makampuni makubwa na baadaye kuondoa mabango madogo na kwamba hatua zaidi za kisheria zitachukuliwa dhidi yao pamoja na kupelekwa mahakamani.
“Mabango tunayovunja na kuyaondoa ni yale yanayodaiwa kodi kwa muda mrefu na manispaa, zoezi hili ni la siku  14 na tutawapeleka mahakamani kwa wale ambao pamoja na hili zoezi hawatalipa,” alisema Henerico.
Alisema mabango hayo ni yale ya makampuni makubwa, watu binafsi na mashirika, ambapo alisema baadhi ya watu binafsi wakati wa zoezi hilo walianza kulipa huku wakikubali kulipa na faini zao kwa wakati huohuo
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa