Home » » CHADEMA: Mwekezaji Mtibwa anyang’anywe kiwanda

CHADEMA: Mwekezaji Mtibwa anyang’anywe kiwanda

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeitaka serikali kumnyang’anya mwekezaji wa kiwanda cha sukari Mtibwa rasilimali hiyo kutokana na kushindwa kuwalipa wakulima na wafanyakazi madai yao.
Diwani wa Mtibwa, Luka Mwakambaya (CHADEMA), alitoa kauli hiyo ikiwa ni siku chache baada ya Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Antony Mtaka, kusimamisha uzalishaji wa kiwanda hicho hadi wakulima na wafanyakazi hao watakapolipwa malipo yao sh bilioni 1.9.
Akizungumza na Tanzania Daima jana, Mwakambaya ameijia juu Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na watendaji wake, kwamba hawana uchungu na maisha ya wananchi wanaonyanyasika ndani ya nchi yao, kutokana na kushindwa kumuadabisha mwekezaji huyo.
“Wananchi wanashindwa kulipa matibabu ya ndugu zao hospitali ya Bwagala, wanafunzi wameshindwa kupelekwa shule, wanashindwa kuvaa na kujikimu wenyewe kwa mahitaji, kutokana na mwekezaji kuhodhi malipo ya wakulima wadogo wa miwa na mishahara ya wafanyakazi.
“Ninafanya upembuzi yakinifu wa majina ya wastaafu zaidi ya 110 waliokufa bila kupata mafao na haki zao stahili, huku wengine wakiwa wamelipwa kati ya shilingi 5oo,ooo au milioni moja ijapokuwa wamefanya kazi zaidi ya miaka 32 na wengine kufukuzwa bila sababu,” alisema Mwakambaya.
Alisema katika ahadi aliyoitoa Meneja wa kiwanda, Hamad Yahaya, siku ya mkutano wa hadhara baina ya Mkuu wa Wilaya, Mtaka na wakulima na wafanyakazi, aliahidi kuingiza  fedha hizo, lakini fedha iliyoingizwa kwenye chama kimoja cha wakulima ni sh milioni 70.
Alisema hali hiyo ni dharau na matusi kwa wakulima na wafanyakazi wanaoteseka na familia zao nchini kwao, kana kwamba wako Somalia, hivyo akadai anasikilizia kikao cha kesho na Mtaka kitakuwaje, vinginevyo wataiomba polisi iwalinde mlangoni kwa mwekezaji watakakoweka mikeka
Chanazo;tanzniaDAIMA 

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa