Wananchi hao walitoa kauli hiyo juzi wilayani hapa walipozungumza na waandishi wa habari kuhusiana na suala hilo.
Katika ziara hiyo ya CCM ikiongozwa na Katibu Mkuu wake, Abdulrahman
Kinana, mawaziri waliotajwa kuwa mizigo ni pamoja na Christopher Chiza
(Kilimo, Chakula na Ushirika), Naibu wake, Adam Malima, Dk. Shukuru
Kawambwa (Elimu), Profesa Jummane Maghembe (Maji).
Akizungumza kwa niaba ya wenzao, Emanuel Mkalimoto, alieleza katika
ziara yake wilayani Ulanga iliyofanyika Agosti mwaka jana, Katibu Mkuu
huyo wa CCM aliyekuwa ameambatana na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape
Nnauye, walisifia utendaji kazi wa Waziri Kombani.
Alisema viongozi hao walieleza wazi kati ya mawaziri wachapa kazi
katika Serikali ya Rais Jakaya Kikwete, Waziri Kombani ni mmojawapo kuwa
amekuwa akitekeleza majukumu yake ipasavyo, lakini anashangazwa na yeye
kuhusishwa kuwa ni miongoni mwa mawaziri mizigo.
Naye Stanley Mhina, alisema katika ziara hiyo, viongozi hao walimsifu
mbunge huyo kuwa ni mmoja wa watekelezaji wa ilani ya chama hicho
katika Jimbo la Ulanga Mashariki kwa kuwaletea maendeleo na hivyo
kupunguza kasi ya wapinzani kulinyemelea jimbo hilo.
“ Binafsi nilikuwepo katika ziara nzima ya viongozi wetu wa juu wa
CCM, walikuwa wakisifu utendaji wa Waziri Kombani kuanzia wizarani na
katika jimbo letu kuwa ni mfano wa kuigwa baada ya kuona maendeleo sasa
tunashangazwa leo, je, wamesahau kauli zao?” alihoji Mhina.
Alipotafutwa kutoa ufafanuzi huo, Waziri Kombani alikataa kulizungumzia suala hilo kwa madai sasa lipo katika mamlaka nyingine.
Chanzo;Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment