Hivi karibuni Rais Jakaya Kikwete aliikataa taarifa ya watu
walioathirika na mafuriko yaliyotokea eneo la Dumila katika Wilaya za
Kilosa na Mvomero mkoani Morogoro.
Wakati hayo yakitokea, naye Mkuu wa Mkoa wa Mbeya
Abass Kandoro aliikataa taarifa ya fedha zilizotumika kwenye ujenzi wa
mabwawa mawili wilayani Mbozi.
Taarifa iliyokataliwa na Rais Kikwete ilikuwa
ikitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera ambayo bila shaka
iliandaliwa na jopo la viongozi wa mkoa na wilaya husika wakiwamo wakuu
wa wilaya na wakurugenzi.
Katika taarifa yake Bendera alisema wananchi
12,472 walipoteza makazi, na kuongeza kwamba nyumba 1,141 zilibomoka na
nyumba zingine 2,755 ziliingiliwa na mafuriko.
Bila shaka sentensi hiyo hapo juu ina utata mwingi. Ina utata kwa sababu haijawa wazi kwa kutamka ukweli wa mambo yalivyo.
Bila shaka sentensi hiyo hapo juu ina utata mwingi. Ina utata kwa sababu haijawa wazi kwa kutamka ukweli wa mambo yalivyo.
Kwa msomaji yeyote wa takwimu hapo juu angependa
kujua tofauti ya kati ya wakazi 12,472 kupoteza makazi na takwimu ya
nyumba 1.141 kubomoka.
Baadhi ya maswali ya kujiuliza ni je wakazi 12,472
waliopoteza makazi, nyumba zao zipo? Pili je nyumba 1,141
zilizobomolewa zilikuwa za nani?
Mkuu wa mkoa anasema nyumba 2,755 ndizo zilizoingiliwa na mafuriko, sasa ziko salama ama zilibomolewa?
Hayo ni baadhi tu ya maswali ambayo kwa kweli
nadhani alijiuliza sana Rais Kikwete na hatimaye kuamua kuikataa taarifa
ya mkuu wa mkoa.
Kimsingi taarifa ingechanganya mambo muhimu
yakiwamo ya vijiji vilivyoathirika vina watu wangapi, na walioathirika
ni wangapi, nyumba zilizobomoka na idadi ya wamiliki wa nyumba na
familia zao.
Hivyo nasisitiza kwamba kwa taarifa zenye utata
kama hizo kutolewa mbele ya kiongozi mkuu wa nchi ni fedheha na kwa
kweli wahusika lazima wajiulize sababu za kutokea mambo hayo.
Cha msingi, hata kama waandaaji wapo, lakini
kiongozi atakayewasilisha taarifa mbele ya watu wengine lazima
ajiridhishe kwa kuhakikisha yaliyoandikwa yana ukweli mtupu.
Tabia za kusoma hotuba ama taarifa mbele ya
hadhira zilizoandikwa na watu wengine bila ya kuzipitia kwanza zina
madhara makubwa.Baadhi ya madhara ni kuaibika na kudhalilika mbele ya
jamii kama ilivyotokea. Hivyo msomaji lazima awe makini zaidi ya
aliyeaandaa.
Hali kadhalika wapo watendaji ambao kwa makusudi wanaandaa
taarifa za kupotosha kwa lengo la kutaka kuongeza idadi ya waathirika
ili misaada ikitolewa wafaidi na waathirika hewa.
Utata kama huo umejitokeza mara kadhaa kwenye maeneo ya majanga na kuisababishia Serikali hasara.
Pia wapo watendaji wa Serikali ambao kwa makusudi
wanaandaa taarifa za kuwasomea wakuu wa wilaya ama mikoa na hata
mawaziri zikiwa na kasoro nyingi.
Wengine wanatoa taarifa za uongo hata masuala
muhimu kwa jamii zikiwamo za kujua ukweli kama wananchi wanakabiliwa na
njaa , kujua ukweli kuhusu magonjwa yanayosumbua wilaya ama mkoa, kujua
ukweli wa kuwapo mauaji ya kutisha.
Wapo viongozi wa halmashauri ama wilaya ambao
wanatoa taarifa nzuri kuhusu elimu, maji na hata afya, lakini
ukichunguza ukweli ni aibu tupu.
Kwa mfano hivi karibuni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya,
Kandoro naye alilazimika kuikataa taarifa iliyohusu matumizi ya fedha za
kujenga mabwawa katika vijiji viwili wilayani Mbozi.
Kandoro alifika Mbozi ambako pamoja na mambo
mengine alipokea taarifa za ujenzi wa bwawa la maji katika Kijiji cha
Iyula na la Kijiji cha Msia.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment