Home » » CCM Moro yatetea mawaziri

CCM Moro yatetea mawaziri

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Morogoro, kimesema wabunge wake waliopo kwenye nyadhifa za uwaziri sio mizigo kwa kuwa wameonekana kufanya kazi vizuri.
Wabunge wa Mkoa wa Morogoro ambao wamo katika nyadhifa hizo ni Mbunge wa Ulanga Mashariki, Celina Kombani ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Mbunge wa Mvomero, Amos Makalla ambaye ni Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana kuhusu utekelezaji wa ilani ya uchaguzi kwa wabunge wa mkoa huo, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Morogoro, Innocent Kalogerezi, alisema mawaziri  hao wameonyesha utendaji mkubwa tangu walipoteuliwa kushika nyadhifa hizo.
Alisema kutokana na hali hiyo ndiyo maana katika ziara ya Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Abdulrahman Kinana katika mikoa ya kusini hawakutajwa mawaziri wanaotoka Morogoro katika orodha ya mawaziri mizigo.
Alisema kuwa Waziri Kombani ni mmoja wa wabunge wa mfano wa kuigwa katika Mkoa wa Morogoro kutokana na utendaji wake katika wizara zote alizopewa nafasi ya kuongoza na Rais Jakaya Kikwete.
Akimzungumzia Waziri Makalla, alisema kuwa naye ni mmoja wa mawaziri wanaofanya vizuri licha ya kuwa na kipindi kifupi tangu ateuliwe kushika nafasi hiyo.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa