Hali ya usalama haijawa shwari katika
Wilaya ya Mvomero, mkoani Morogoro kati ya wakulima na wafugaji baada ya kundi
la vijana wafugaji kuvamia gari walilopanda wakulima na kuwapa vipigo na
kuwajeruhi.
Katika tukio hilo, mfugaji mmoja alifariki dunia baada ya kugongwa na gari lililokuwa limewabeba wakulima waliokuwa wakitoka kuandaa mashamba eneo la Mgongola.
Katika tukio hilo, mfugaji mmoja alifariki dunia baada ya kugongwa na gari lililokuwa limewabeba wakulima waliokuwa wakitoka kuandaa mashamba eneo la Mgongola.
Tukio hilo limetokea juzi wakati
wakulima hao wakiwa ndani ya gari aina ya Isuzu baada ya kufika eneo la
Kambala na ghafla kusimamishwa na kundi la morani wa Kimasai.
Mmoja wa wakulima hao, Omar Hamad, alisema wakiwa ndani ya gari hilo yeye na wenzake watano walisimamishwa, lakini dereva wao alitakaa na alipoendelea mbele alikuta magogo yamepangwa barabarani na kulazimika kusimama.
Alisema ghafla kikundi cha morani kiliwavamia na kuanza kuwashambulia kwa kutumia silaha mbalimbali na baadhi yao kujeruhiwa na kuamua kukimbilia porini kuokoa maisha yao.
Alisema baada kuona mashambulizi yanaongezeka, dereva aliamua kulitoa gari hilo kwa kasi na ndipo mbele yake alikutana na pikipiki iliyokuwa inakuja mbele yao , lakini ilipoteza mwelekeo na gari kuigonga na kusababisha kifo cha dereva wa pikipiki hiyo ambaye alikuwa mfugaji.
Kaimu Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Morogoro, John Laswai, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa lilitokea jioni katika kijiji cha Kambala.
Mmoja wa wakulima hao, Omar Hamad, alisema wakiwa ndani ya gari hilo yeye na wenzake watano walisimamishwa, lakini dereva wao alitakaa na alipoendelea mbele alikuta magogo yamepangwa barabarani na kulazimika kusimama.
Alisema ghafla kikundi cha morani kiliwavamia na kuanza kuwashambulia kwa kutumia silaha mbalimbali na baadhi yao kujeruhiwa na kuamua kukimbilia porini kuokoa maisha yao.
Alisema baada kuona mashambulizi yanaongezeka, dereva aliamua kulitoa gari hilo kwa kasi na ndipo mbele yake alikutana na pikipiki iliyokuwa inakuja mbele yao , lakini ilipoteza mwelekeo na gari kuigonga na kusababisha kifo cha dereva wa pikipiki hiyo ambaye alikuwa mfugaji.
Kaimu Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Morogoro, John Laswai, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa lilitokea jioni katika kijiji cha Kambala.
Alisema tayari Jeshi la Polisi limetuma askari katika eneo
hilo kwa ajili ya kuwasaka morani hao.
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment