Home » » Chagonja awasili ‘uwanja wa mapambano’Chagonja awasili ‘uwanja wa mapambano’

Chagonja awasili ‘uwanja wa mapambano’Chagonja awasili ‘uwanja wa mapambano’

Mvomero.Mkuu wa Operesheni wa Polisi, Paul Chagonja amewasili eneo la mapigano kati ya wakulima na wafugaji vijiji vya Hembeti na Kambara, Wilaya ya Mvomero, yaliyosababisha mauaji ya watu sita.
Hata hivyo, Chagonja baada ya kuwasili aliwataka wananchi kumaliza migogoro kwa amani na utulivu, huku akiwasisitiza kutumia njia ya mazungumzo badala ya kujichukulia sheria mkononi.
Chagonja aliyeongozana na maofisa wengine kutoka Makao Makuu ya Polisi Dar es Salaam, alisema kutokana na vurugu hizo watu sita wamefariki dunia na kujeruhi 30.
Alisema polisi wameimarisha ulinzi na kwamba, hali kwa sasa ni tulivu hivyo wananchi waendelee kuimarisha umani kufuata sheria kupata haki zao.
Aliongeza kuwa licha ya kusababisha vifo na majeruhi, vurugu hizo zimeathiri shughuli za uchumi na huduma za jamii kusimama.
kama shule hasa ukizingatia kwa sasa wanafunzi wa kidato cha nne wanafanya mitihani na kwamba katika vijiji hivyo wapo wanafunzi wa kidato cha nne ambao naweza kushindwa kwenda kufanya mitihani yao wakihofia vurugu zinazoweza kujitokeza wakiwa shuleni ama wakati wa kwenda shule.
Awali akizungumzia vurugu hizo, Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile alisema kuwa tukio hilo lilitokea Novemva 4 mwaka huu saa 10:00jioni baada ya ng’ombe 300 wa Semwako Mtunda ambaye ni mfugaji wa jamii ya kimasai kutoka kitongoji cha Mpapa Hembeti kuingiza ng’ombe katika mashamba ya wakulima wanne na kuharibu mazao mbalimbali.
Alisema ng’ombe hao walichukuliwa na kikundi cha ulinzi wa jadi cha Mwano na kupelekwa kwenye kijiji cha Hembeti ,wakiwa katika ofisi ya kijiji wakiendelea na majadiliano kwa pande zote mbili kikundi cha ulinzi wa jadi cha Mwano kugoma na kudai kupewa kiasi cha sh.3 milioni na mmiliki wa ng’ombe hao alikubali kulipa lakini walinzi kugomea kiasi hicho cha fedha.
Alisema wakati wakiendelea na madailiajo hayo ndipo walipotokea wafugaji wa jamii ya kifugaji wakiwa na silaha za moto kwa ajili ya kutaka kuchukua mifugo na katika harakati hizo za mapigano kulipelekea majeruhi tisa na kupelekea mtu mmoja Yusuf Mbutu mkulima wa kijiji cha Mkindo kufariki dunia majira ya jioni
Ilielezwa kuwa Novemba 6 mwaka huu, saa 4:00 asubuhi kulitokea mapigano mengine katika eneo la kijiji cha Mpapa-Kigulukilo kati ya kikundi cha Ulinzi wa jadi cha Mwano na wafugaji wa kimasai hali iliyopelekea kifo cha watu watano na majeruhi 28 kati yao wawili wafugaji na watatu kutoka kikundi cha ulinzi wa jadi cha Mwano.

Chanzo;Mwananhi

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa