Home » » Bodaboda za kilimo zaja

Bodaboda za kilimo zaja



KAMPUNI ya General Business (GB) ya mjini hapa, imeingiza aina mpya ya pikipiki kutoka nchini China ambazo zitatumika kwa ajili ya wakulima kuongeza uzalishaji wa zao la mpunga na mahindi.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, Mkurugenzi Mtendaji wa GB Morogoro, Peter Mpembwa, alisema kampuni hiyo imeamua kuingiza pikipiki hizo ili kumpunguzia gharama za uzalishaji na kumwezesha mkulima kuzalisha kwa tija.
Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo, pikipiki hizo ikiwemo aina ya GN, Escort na Elegant, ambazo tayari zipo mjini hapa, zimeundwa katika muundo wenye uwezo wa kukabiliana na mazingira  ya vijijini kwa ajili ya kilimo.
‘‘Baada ya kuona serikali imekuja na sera ya 'Kilimo kwanza' yenye dhamira ya kuinua kilimo nchini, GB ilifanya mazungumzo na kampuni za nje ikiwemo Kampuni ya  China ya GS-Group ili tupate nyenzo rahisi katika kumpunguzia gharama mkulima...wakaja na aina hii ya pikipiki,” alisema Mpembwa.
Kuhusu mpango mkakati wa kampuni hiyo, Mpembwa alisema zaidi ya ekari 500 zinatarajiwa kuanza kutumika kuzalisha zaidi ya tani 300 za mpunga ili kuuwezesha mkoa kuzalisha mpunga utakaotosheleza mahitaji ya ya chakula nchini.

Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa