Home » » UVCCM,MADIWANI MVOMERO WALUMBANA

UVCCM,MADIWANI MVOMERO WALUMBANA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
JUMUIYA ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wilayani Mvomero, Morogoro, imeingia kwenye malumbano na Baraza la Madiwani baada ya mwenyekiti wa jumuiya hiyo kuwaita madiwani ‘mizigo, wazee, viwete na hawana tija’ ndani ya chama.
Hali hiyo ilijitokeza baada ya Mwenyekiti wa umoja huo, Paschal Boga, katika kikao cha Baraza la Vijana wa chama hicho kilichoketi Februari 15, mwaka huu kuwatuhumu madiwani wa halmashauri hiyo kuwa ni mzigo kwenye chama kwa kushindwa kutekeleza ilani ya chama na kutetea maslahi ya wananchi.
Mmoja wa wajumbe kwenye kikao hicho ambaye hakutaka jina litajwe, alisema malumbano hayo yaliyosababisha wajumbe hao kurushiana maneno makali na vitisho, yalianza baada ya baadhi ya wajumbe kuhoji zilizopo fedha asilimia tano ya pato la halmashauri zinazotakiwa kupelekwa kwa makundi ya vijana na wanawake.
Alisema baada ya kuibuliwa kwa hoja hiyo na kumlazimu ofisa utamaduni wa halmashauri hiyo kusema fedha zimekuwa zikitolewa tangu mwaka 2009 bila takwimu, wajumbe walipinga wakimtaka alete takwimu hizo kwa kuwa kundi hilo limetelekezwa kwa kukosa fursa ya uwezeshwaji.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Jonas Zeeland, alisema hali hiyo ipo ila tayari madiwani wameamua kumwandikia barua katibu wa CCM wilaya ili amshugulikie ofisa huyo.
“Sisi Baraza la Madiwani tumekubaliana kumpa siku 14 athibitishe kwetu na ndani ya chama kauli yake hiyo ya kibaguzi ikiwemo uzembe wetu vikaoni,” alisema Zeeland.
Alisema madiwani wamesikitishwa na kauli hiyo inayowakatisha tamaa ikilinganishwa takribani mwezi mmoja uliopita CCM ikiwakilishwa na wenyekiti wote akiwemo Boga, ilitoa hati kwa madiwani kushukuru dhidi ya utumishi bora ndani ya halmashauri.
Zeeland aliongeza kuwa halmashauri imejipanga kuhakikisha wanapata hati safi kwa mara ya kwanza toka ianzishwe 2003 na hiyo inatokana na kazi iliyofanywa na madiwani waliojitoa muhanga kwa kuisafisha halmashauri, ikiwemo kuwaondoa na kuwashitaki watendaji waliokuwa kikwazo cha maendeleo.
Chanzo:Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa