Home » » Mwenyekiti wa NEC awataka Wasimamizi wa Uchaguzi kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za Uchaguzi

Mwenyekiti wa NEC awataka Wasimamizi wa Uchaguzi kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za Uchaguzi

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
AQO
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi( NEC) Jaji (R) Semistocles Kaijage (kushoto) akisalimiana na Msimamizi wa Uchgauzi wa Jimbo la MorogoroMjiniBw. John Mgalula wakati alipotembelea na kufuatilia mwenendo wa uchgauzi wa Kata ya Kiwanja cha Ndege katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, inayotarajia kufanya Uchaguzi Mdogo tarehe 22 Januarimwaka 2017.Picha na Hussein Makame-NEC-Morogoro.
……………..
Hussein Makame, NEC- Morogoro
Mwenyekitiwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji (R) Semistocles Kaijage amewatakawasimamizi wa Uchaguzi mdogounaotarajiwakufanyikaJumapili hii kuwa wahakikishewanazingatiaSheria, Kanuni na Taratibu ili kuepushakubatilishwa kwa Uchaguzi.
Jaji (R) Kaijage aliasema hayo baada ya kupokea taarifa ya mwenendowa Uchaguzi Mdogo wa Kata ya Kiwanja cha Ndegeiliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mogoro kutoka kwa Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la MorogoroMjini.
Alisemakutozingatiwakwataratibu za Kisheria za Uchaguzi kunawezakusababishakubatilishwa kwa Uchaguzi mzima na hatimayekuisababishiaSerikalihasarakubwa, hivyo amemkumbushaMsimamizi wa Uchaguzi kuhakikisha wanafuataSheria.
“Kwa kuwa miongozo yote mnayoya Sheria, KanuninaTaratibuza Uchaguzi, hakikishenimnatekelezakilawajibu wa Kisheria katika zoezi hilikwa sababu kutozingatiwakwataratibu za Kisheriakunawezakusababisha Uchaguzi ukabatilishwa” alisemaJaji (R) Kaijage.
Akitoa taarifa ya mwenendowa Uchaguzi Mdogo wa Udiwani Kata ya Kiwanja cha Ndege,Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la MorogoroMjini, Bw. John Mgalula, alisemamaandalizi ya Uchaguzi yanakwendavizuri na wanakamilishaujenzi wa baadhi ya vituo vya kupigiakura.
Alisemakamati za maadilizimeshaundana hadi wiki iliyopitazilikuwahazijapokeamalalamikoyoyoteingawajuziJumatatuwalitarajiakukutananawawakilishi wa vyama vya CHADEMA, CUF na CCM ili kuwakumbusha kuzingatia maadili ya Uchaguzi.
Kwa upande wake Mkurugenzi waHuduma za Kisheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bw. Emmanuel KawishealimkumbushaMsimamiziwa Uchaguzi kuwafahamisha mapema watendaji wa vituo kuhusumalipo ya poshoya kazi yao ili kuepushasintofahamu.
Alisemawakati wa semina kwa wasimamizi wa vituo na makaraniwaongozaji ni vyema Msimamizi wa Uchaguzi akawatangazia watendaji hao kuhusu malipo ya posho kwani inawezakusababishavurugu na uharibifu wa vifaaiwapohawataridhika na malipo husika.
NayeMkuuwa Kanda ya Kati ya Uchaguzi wa Tume, Bi.SaadaKangetaalimsisitizaMsimamiziwa Uchaguzi kuwakumbushawasimamizi wa vituo au wasaidizi wao watumiemamlakamliyopewavizuri kwa sababu baadhi yao wanazitumiavibaya.
“Kuna wakatiinatokea baadhi ya wasimamiziwanapopewamamlaka ya kusimamiakituoanajionaanamamlaka ya kumuoneamtukwa sababu waligombana.Hivyowakumbusheniwatumiemamlakawaliyopewavizuri kwanikilamamlakainaSheria na Sheriazipo na zinatakiwakufuatwa” alisema Bi. Kangeta.
Alimkumbushamsimamiziwa Uchaguzi kuwatangaziawapigakurakuhakikimajina yao kwenye Daftari la Wapiga kuralililobandikwa kwenye vituo vya kupigiakura kwani kutofanya hivyo kunawezakusababishausumbufu siku ya kupigakura.

 

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa