Home » » Mazao ya Uhandisi Jeni kupewa msukumo mpya

Mazao ya Uhandisi Jeni kupewa msukumo mpya

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

KATIBU Mkuu wa Wizara Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dk Florens Turuka amesema Serikali iko tayari kushirikiana na watafiti wa kilimo kuandaa mazingira yatakayowezesha nchi kuruhusu uzalishaji wa mazao yanayotokana na Uhandisi Jeni (GMO).
Akizindua ripoti ya hali ya biashara kwa mazao ya baiteknolojia jana mjini hapa, Dk Turuka alisema lengo la kuruhusu mazao hayo ni kufanya kilimo kiwe na tija kubwa kutokana na sekta kukabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukame na magonjwa.
“Tanzania hatuwezi kukwepa matumizi sahihi ya teknolojia, lazima tuhakikishe tunakuwa na matumizi sahihi na kuondoa wasiwasi ndani ya jamii yetu,” alisema Dk Turuka.
Alisema ipo haja ya watafiti na serikali kufanya kazi kwa karibu ili kutoa elimu juu ya upotoshaji unaofanywa na wanaharakati kuhusu mazao ya GMO.
Dk Turuka alisema sheria na kanuni zilizokuwepo awali zimerekebisha na sasa utafiti wa mazao ya GMO umeruhusiwa nchini.
Alisema serikali inaendelea kuandaa miongozo mbalimbali ambayo itasimamia mazao ya baiteknolojia. Alitoa mwito kwa watafiti hao kufanya karibu na Serikali ili kuielimisha jamii juu ya matumizi sahihi ya teknolojia ya GMO.
Chanzo Gazeti La Habari Leo

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa