Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa
Makame Mbarawa, amewataka makandarasi waliosimamisha kazi, kuendelea na
ujenzi baada ya serikali kuanza kuwalipa madai yao.
Profesa Mbarawa aliyasema hayo jana akiwa wilayani Mvomero,
Morogoro, baada ya kukagua ujenzi wa barabara ya Magole-Turiani yenye
urefu wa kilomita 48.6.
Prof. Mbarawa alisema serikali imeshalipa makandarasi mbalimbali
Sh. bilioni 400 na itaendelea kufanya hivyo ili kumaliza madeni yao kwa
haraka.
“Hakikisheni mnarejea kazini na kuwapa mikataba ya ajira
wafanyakazi wenu katika kipindi cha wiki mbili kuanzia sasa ili ujenzi
wa barabara na madaraja ukamilike kwa mujibu wa mkataba hivyo kuondoa
usumbufu kwa watumiaji wa barabara hii,” alisema.
Katika hatua nyingine, Waziri Prof. Mbarawa alikagua karakana ya
ujenzi wa vichwa vya treni mjini Morogoro na kumtaka mkandarasi
anayekarabati vichwa hivyo kufanya kazi hiyo kwa haraka na kutoa kazi
zingine kwa Watanzania ili kuwajengea uwezo wa kazi hizo.
Aidha, Profesa Mbarawa aliwataka wafanyakazi wa Kampuni ya Reli
Tanzania (TRL), kufanya kazi kwa ubunifu, uadilifu na uwazi ili kufufua
hadhi ya kampuni hiyo ambayo ni muhimu kwa uchumi wa nchi.
Alisema takribani asilimia 96 ya mizigo inayoshushwa katika Bandari
ya Dar es salaam husafirishwa kwa njia ya barabara, hivyo ni jukumu la
TRL kuhakikisha inapata mizigo ya kutosha ya kusafirisha.
Naye Mbunge wa Mvomero, Suleiman Sadik, aliiomba serikali kumalizia daraja la Diwale lenye urefu wa mita 75 ili liweze kupitika.
CHANZO:
GAZETI LA NIPASHE
0 comments:
Post a Comment