Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Magreth Kinabo –maelezo
30/09/2015
Serikali imemtaka
kila mwanajamii kutafakari haki ambazo wazee wanastahili na kuweka mipango ya
makusudi katika kuwawezesha kuzipata haki hizo.
Kauli hiyo
imetolewa leo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii,Dkt, Donan Mmbando
kupitia tamko la wizara hiyo kuhusu
maadhimisho ya siku ya kimataifa ya
wazee duniani itakayofanyika kesho Oktoba Mosi ,mwaka huu wilayani Kasulu mkoani Morogoro.
Kauli mbiu
ya mwaka huu ni “Umuhimu Kuwashirikisha Wazee
Kwa Ustawi Endelevu Mijini”.
“Uko umuhimu
kwa jamii yetu kutafakari iwapo tunatambua mahitaji halisi na kuthamini
michango yao kama rasilimali muhimu katika maendeleo ya taifa.
“Tunawashirikisha,
tunawaheshimu na kuwaendeleza kama wananchi wengine na tunaheshimu mila na
desturi nzuri za kuwaenzi wazee hao,” alisema Dkt. Mmbando.
Aliongeza kwamba wazee katika nchi yetu wanayo
nafasi kubwa katika juhudi za kuleta maendeleo. Katika maisha ya kila siku ya
jamii, wazee wanakubalika kuwa ni watoa habari, ujuzi wa mila na desturi, washauri
na wapatanishi. Pia wazee ni walezi wa watoto wadogo,hususan kwa watoto yatima
walioachwa na wazazi wao kutokana na janga la UKIMWI.
“ Natoa wito kwa watendaji wote kwa nafasi zao
mbalimbali hususan wakurugenzi watendaji
Halimashauri za Miji/Manispaa/Wilaya na wakala mbalimbali zinazotoa
huduma kwa wazee ili ziweke mipango inayozingatia haki za wazee na kuimarisha
mifumo ya kinga ya jamii iliyopo ili kuboresha huduma wanayopata,” alisisitiza.
Aidha Dkt.
Mmbando alisema alisema suala la wazee ni mtambuka, hivyo kila idara na asasi
mbalimbali za Serikali na watu binafsi zishiriki katika kuhakikisha kwamba juhudi juhudi za makusudi zinafanywa ili
kuboresha maisha ya wazee.
Alisema Serikali itaendelea kutambua na kuthamini
michango inayotolewa na wazee katika
maendeleo ya taifa letu.
“ Hivyo
nawaomba wazee waendelee kushirikiana na Serikali yao katika kuendeleza
utulivu na amani tuliyonayo na pia
waendelee kuwa kielelezo bora na urithi kwa vijana wetu kwa manufaa ya taifa
letu,” alisema.
Alitoa changamoto kwa vijana kuwa karibu na
wazee ili kujifunza maadili mema toka kwao na kuwajibika kuwahudumia ipasavyo
na kuweka taratibu za kujiwekea akiba kila wanavyopata ikiwa ni sehemu ya
mikakati ya kufanya maandalizi ya maisha kuelekea uzeeni.
0 comments:
Post a Comment