10
wadaiwa kukutwa na silaha, milipuko msikitini, Pia nguo za kijeshi,
mmoja ajeruhi polisi kwa jambia, Wananchi wamuua kwa kumchoma moto.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Leonard
Paul, akiwaonyesha waandishi wa habari (hawapo pichani), milipuko
inayodaiwa kuwa ni ya hatari ambayo iliyokamatwa juzi usiku kutoka kwa
watuhumiwa tisa waliokuwa wamehifadhiwa ndani ya Msikiti wa Suni uliopo
tarafa ya Kidatu wilayani Kilombero.PICHA: MPIGAPICHA WETU
Aidha, mmoja wa watuhumiwa hao anadaiwa kuuawa kwa kuchomwa moto na
wananchi wenye hasira, baada ya kumkata askari polisi shingoni kwa
kutumia jambia.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Leonard Paul, jana alitoa
taarifa kwa vyombo vya habari kwamba, tukio hilo lilitokea tarafa ya
Kidatu, wilaya ya Kilombero.
Kamanda Paul alimtaja mtuhumiwa aliyeauwa kuwa ni Hamad Makwendo, mkazi wa Manyasini Ruaha, tarafa ya Kidatu, wilaya ni humo.
Alidai kuwa tukio hilo lilitokea Aprili 14, mwaka huu, saa 3:30 usiku, katika kitongoji cha Nyandero.
Kwa mujibu wa Kamanda Paul, mtuhumiwa aliyeuawa alikuwa kiongozi wa wenzake waliotiwa mbaroni na jeshi hilo.
Alisema siku ya tukio polisi walipata taarifa kwamba kuna watu
wanajihusisha na uhalifu na kuanza kuwafuatilia kwa muda, lakini
walikuta tayari wakiwa wameshaondoka kuelekea maeneo yasiyojulikana.
Kamanda Paul alidai polisi walipata taarifa kuwa watu hao walitumia usafiri wa bajaji.
Alisema wakati wakiendelea kuwafutilia, walikutana na bajaji moja ikiwa na abiria mmoja na kuisimamisha.
Kamanda Paul alisema bajaji hiyo iliposimama, Hamadi ambaye ni marehemu, aliruka na kuanza kukimbia.
Alidai askari mwenye namba F .3323 Koplo Nasoro alianza kumkimbiza
na alipomkaribia, mtuhumiwa huyo alichomoa jambia na kumkata askari huyo
shingoni ambaye alivuja damu nyingi.
Kamanda Paul alidai kuwa askari mwingine mwenye namba E9245 Koplo
Chomola, aliyekuwa nyuma, alifanikiwa kumpiga mtuhumiwa risasi mguuni.
Alidai kuwa mtuhumiwa huyo alipoanguka chini, wananchi wenye hasira
walifika eneo hilo na kuanza kumshambulia na kisha kumchoma moto.
Kutokana na hali hiyo, alidai kuwa walilazimika kuongeza kikosi cha
askari kutoka mkoani ili kuendesha operesheni ya kuwasaka watuhumiwa
wengine.
Kamanda Paul alidai kuwa wakiwa kwenye operesheni hiyo walipata
taarifa kuwa baadhi ya watuhumiwa walikuwa katika msikiti wa Suni,
uliopo eneo la Kidatu.
Alidai kuwa askari walifika katika msikiti huo na kuomba viongozi
wake kwa kushirikiana na wa serikali kuwatoa watu wote waliokuwa
msikitini ili kubaini watu wanaotiliwa shaka juu ya kuhusika na matukio
ya kihalifu.
Kamanda alidai kuwa waumini wote walitakiwa kutoka nje ya msikiti wakiwa na mikoba yao.
Alisema baada ya hapo, polisi walianza kufanya ukaguzi na
kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa 10 wakiwa na vifaa mbalimbali vya
kufanyia uhalifu.
Kamanda Paul alidai vitu vilivyokutwa katika mikoba ya watuhumiwa
hao ni pamoja na milipuko 30, bendera nyeusi yenye maandishi ya Mungu
mmoja, nyaya za kulipulia milipuko (detonators), majambia, bisibisi,
vifaa vya kuficha uso (masks), sare za jeshi, misumeno ya chuma, spana,
madaftari na vitabu mbalimbali vikiwamo vya stakabadhi.
Alidai kuwa mbali na vitu hivyo, pia marehemu alikutwa na risasi
sita, tano zikiwa za bunduki aina ya SMG na moja ya bunduki aina ya Mark
IV pamoja na ‘detonators fuse’ mbili zikiwa katika mfuko mdogo wa
jeshi.
Kamanda Paul alidai askari aliyejeruhiwa alipoteza damu nyingi na
kwamba, alikimbizwa katika Hospitali ya Kiwanda cha Sukari cha Kilombero
na hali yake inaendelea vizuri, huku taratibu za kumhamishia Hospitali
ya Rufaa Mkoa wa Morogoro zikiendelea kushughulikiwa.
NIPASHE jana iliwasiliana na imamu wa msikiti unaotajwa bila mafanikio.
CHANZO:
NIPASHE
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment