Home » » FOMU UCHAGUZI CHADEMA MORO KUTOLEWA LEO

FOMU UCHAGUZI CHADEMA MORO KUTOLEWA LEO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoani hapa, kimetangaza kuanza kutoa fomu leo kwa wanachama wanaotaka kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika ngazi ya wilaya na jimbo huku kikitahadharisha vitendo vya rushwa.
Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Chama cha Waandishi wa Habari mkoani hapa (MOROPC), Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Morogoro, Ngonyani Ngonyani, alizitaja nafasi zinazowaniwa kuwa ni mwenyekiti, katibu, katibu mwenezi, mweka hazina, wajumbe wa kamati tendaji na mabaraza yote ya chama ikiwemo vijana, wanawake na wazee.
Alisema fomu hizo zinatolewa kwa gharama ya sh 10,000 kwenye ofisi zote za kata, wilaya na kwenye tovuti ya chama na zinatakiwa kuwa zimerudishwa Agosti 7 saa 10 jioni kisha mchujo utafuata Agosti 8 na 9.
Kwa mujibu wa katibu huyo, mkoa una wilaya saba na majimbo 10, na kwamba tofauti na chaguzi zilizopita, sasa hivi makatibu watajaza fomu kama nafasi nyingine na zitapelekwa taifani kupitiwa na kuteuliwa na kamati kuu ya uteuzi.
“Uchaguzi wetu ni tofauti na vyama vingine, maana hatuna kampeni, mpaka sasa tayari tunashirikiana na makachero wetu na Takukuru kudhibiti udanganyifu, lakini kama haitoshi baada ya mchujo Agosti 9, Agosti 10 tunakutana ukumbini na kila mtu atajinadi na kuchaguliwa moja kwa moja,” alifafanua.
Alisema wote watakaokamatwa kwa rushwa au kuwa na harufu ya rushwa, majina yao yataondolewa moja kwa moja kwenye kinyang’anyiro na kuburuzwa kwenye nyombo vyenye mamlaka vikiwemo vya sheria.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa