Home » » 'VIMEMO' CHANZO MIGOGORO YA ARDHI

'VIMEMO' CHANZO MIGOGORO YA ARDHI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

CHANZO cha migogoro ya ardhi isiyokwisha katika vijiji mkoani Morogoro, kimebainika kuchochewa na vijikaratasi na vibali vyenye maagizo kutoka kwa vigogo wenye mamlaka serikalini.
 vikitaka wananchi na viongozi wa vijiji kutopuuza badala yake watekeleze yaliyo kwenye vikaratasi hivyo.
Hayo yaliibuliwa mwishoni mwa wiki kwenye mafunzo ya siku tatu kuhusu sera na sheria za ardhi kwa wenyeviti,watendaji,makundi maalumu wakiwemo wakulima na wafugaji wa vijiji vya Kata ya Maguha na Magubike, wilayani Kilosa yaliyoandali na asasi ya Dira Theatre Group na Foundation for civil society .
 Madai  hayo yalisababisha Diwani wa Magubike, Ernest Chilolo aliyekuwa mgeni rasmi akishirikiana na Ofisa Mtendaji kata hiyo, James Mnghondwa, kuhamaki na kupiga marufuku kwa watendaji na wenyeviti hao kupokea na kufuata maagizo hayo kinyume na sheria, taratibu na kanuni za nchi husuasani ardhi.
Katika madai hayo, baadhi ya washiriki hao wakiwemo mfugaji Lethon Mhumbuja wa Magubike na Mwenyekiti wa Inyunywe Antho Nyangasi, walisema kutokana na kuviheshimu vikaratasi hivyo, wamejikuta maeneo yao yamejaa migogoro isiyoisha kila kukicha.
“Unakuta mtu anakibali ‘hati’ kutoka wizarani inaonyesha amepewa karibu nusu ya kijiji na maagizo yanamtaka Mwenyekiti atekeleze…manafikiri tufanyeje! Ndio unakuta kunaibuka vurugu maana wakati mwingine kapewa hadi eneo lenye huduma kama maji, shule au huduma ya afya,”alisema Mhumbuja.
Walisema migogoro katika vijiji mkoani Morogoro inatokana na wananchi kutoshirikishwa katika utwaaji maeneo, uwekezaji usio na tija, vijikaratasi vitokanavyo na ubabe na nafasi walizonazo vigogo maofisini na uelewa mdogo walionao viongozi wa vijiji na wanachi juu ya masuala ya ardhi.
Walisema sababu nyingi ni umasikini walionao wanachi ambao umekuwa kichocheo kikubwa cha uuzwaji ardhi bila kufuata misingi na taratibu yenye tija kwao na jamii zinazowazunguka.
Diwani Chilolo na Mtendaji kata Mnghondwa mbali na kupiga marufuku kupokea vijikaratasi hivyo, waliwataka viongozi hao wa vijiji kuanza kuainisha maeneo yanayoendeshwa kinyume na sheria na shuguli tofauti, ili wote waliohusika waburuzwe kwenye vyombo vya sheria.
Awali, Mkurugenzi wa Dira, Erasmo Tulo, aliwataka viongozi wa vijiji hadi kata kutojishusha kwenye mamlaka waliyopewa kwa kusimamia kikamilifu sheria, taratibu na kanuni za utumishi bila kujali katika utekelezaji huo anayeumia ni nani.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa