Home » » WAKULIMA WAHOFIA KUZUKA MAPIGANO

WAKULIMA WAHOFIA KUZUKA MAPIGANO

Kilombero. Wananchi wanaoishi vijiji vya Kata ya Utengule, Wilaya ya Kilombero, mkoani Morogoro, wamesema kuna hofu ya kuibuka kwa mapigano baina yao na wafugaji, kutokana na viongozi kuendekeza rushwa.
Wakizungumza kwenye Kijiji cha Mpanga juzi, Mwinuka Kahame na Didram Nuhenga walisema viongozi hao wa Serikali hivi sasa wamegeuza ardhi za vijiji kuwa mtaji wao.
Kahame alisema viongozi hao wanauza ardhi kwa wageni ambayo ni mapori ya vijiji, mashamba na viwanja vya makazi huku wakirejesha kwa kasi wimbi la wafugaji.
“Sasa hivi viongozi wanauza mapori ya vijiji, mashamba na makazi ya wenyeji bila huruma, hawafuati taratibu wala sheria… hakuna mikutano ya kisheria inayoitishwa,” alisema Kahame na kuongeza:
“Wanajua wananchi watahoji na tukikutana nao pembeni tukiwauliza wanatoa majibu machafu.”
Alisema yeye alikuwa na shamba la ekari 10 ambazo alikuwa anazitumia kwa kilimo na makazi, lakini ameshtuka mtu anaweka mipaka na alipouliza viongozi walimweleza amenunua eneo hilo na ana hati miliki.
Naye Nuhenga alisema kwa tathmini waliyofanya vitongoji vya kijiji hicho, wamebaini takriban asilimia 80 ya ardhi ya kijiji tayari imeuzwa na viongozi kwa wageni hususan wafugaji.
Pia, alisema licha ya wananchi kudhulumiwa ardhi yao kwa kunyang’anywa na viongozi wa Serikali, wamekuwa hawasikilizwi wanapopeleka malalamiko yao.
Alisema wafugaji wamekuwa wakilisha mazao ya wakulima, lakini viongozi wa vijiji hawawasilikizi.
Hata hivyo, Mtendaji wa Kijiji cha Mpanga, George Kyelula alikana kuwapo kwa tuhuma hizo na kwamba, yeye ni mgeni ana miezi miwili tangu ahamishiwe hapo.
Alisema hajasikia kitu kuhusu tuhuma hizo na kwamba, hayo ni majungu.
kama hicho wakati mtendaji kata ya Utengule Alex Chawala hakutaka kuonyesha ushirikiano na wanahabari akihoji kwanini wanachi waseme mambo hayo kwenye vyombo vya habari kabla hayajatolewa kibali cha kuzungumza kwenye vyombo vya habari na kudai kuwa hakuna matatizo kama hayo kwenye vijiji vyao licha ya kuwa wananchi wamelalamika
Chanzo:Mwananchi

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa