Home »
» PINDA;SIPATI USINGIZI
PINDA;SIPATI USINGIZI
WAZIRI
Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, amesema mafuriko yaliyotokea Wilaya ya Kilosa,
mkoani Morogoro, yanamfanya akose usingizi hasa baada ya kukatika
Daraja Mkundi ambalo linaunganisha Barabara Kuu ya Morogoro-Dodoma hivyo
kusababisha maji mengi kuingia vijijini.
Bw. Pinda aliyasema hayo
Dar es Salaam jana baada ya kufanya ziara wilayani humo ili kujionea
madhara yaliyotokana na mvua zinazoendelea kunyesha mkoani humo.
Alisema
Serikali imeanza kufanya mikakati ya haraka ili kuhakikisha huduma za
kijamii na kiuchumi zinarudi kama ilivyokuwa awali katika vijiji
vilivyoathirika.
"Haya mafuriko yametokea juzi alfajiri na
kusababisha maji mengi kutokana na mvua zilizonyesha Mikoa ya Manyara na
Arusha, hivyo kusababisha wakazi wa kata za Magole, Belege, Msowelo
kuathirika," alisema.
Aliongeza kuwa, Shule ya Sekondari ya Dakawa, Chuo cha
Ufundi
VETA na Chuo cha Ualimu navyo vimeathiriwa lakini daraja la Mkundi
ndilo linalomnyima usingizi zaidi baada ya kukatika mita 20 upande mmoja
na 40 upande mwingine.
Bw. Pinda alisema, Mkuu wa Mkoa huo Bw. Joel
Bendera amelazimika kubomoa tuta ili kuruhusu maji kutawanyika ambayo
yangeathiri zaidi wananchi kwa upande mmoja
"Hadi sasa, haya
mafuriko yamesababisha kifo cha mtu mmoja, kuharibu nyumba nyingi na
kusababisha hasara kubwa ya mali, mifugo pamoja na mazao.
"Tayari
Serikali imechukua hatua za haraka pamoja na kumuomba Mkandarasi
anayejenga Barabara ya Kilosa kujaza mawe lori 50 katika upande wa
kutokea Morogoro- Dumila na lori 50 za mawe kwa upande wa Dodoma ili
kuyazuia maji," alisema.
Alisema kutokana na hali hiyo, Waziri wa
Ujenzi, Dkt. John Magufuli amelazimika kuweka kambi eneo hilo ili
ukarabati na ujenzi wa barabara hiyo uweze kufanyika haraka na kuruhusu
magari kupita kuanzia leo.
Hadi sasa, msaada wa fedha sh. milioni 50
zimetolewa na Serikali, wahisani pamoja na vitu mbalimbali kama
blanketi, vyakula, dawa, sabuni, mikeka, mahema na vyandarua.
Ka t
ika ha tua ny ing ine , Waandishi Wetu Severin Blasio na Lilian Justice,
kutoka Morogoro wanaripoti kuwa, zaidi ya kaya 500 katika Kijiji cha
Magole, wilayani humo hazina makazi baada ya nyumba zao kusombwa na
maji.
Mvua hizo pia zilisababisha madhara kwa mifugo ambayo ilisombwa na maji, kufa na kuharibu mazao mbalimbali.
Wakizungumza
na Majira jana, wakazi wa kijiji hicho walisema mvua hizo zimewatia
umaskini na hakuna misaada yoyote ya kibinadamu waliyoipata kutoka
serikalini.
Bw. Juma Khamis na Mwanaidi Athuman, walisema hawajui
hatima ya maisha yao hivyo wameiomba Serikali iwapelekee misaada ya
haraka ili kunusuru maisha yao.
Wakati huo huo, zaidi ya watu 7,000
waliopo katika kata tatu zilizopo Tarafa ya Magole, wilayani humo hawana
makazi ya kuishi baada ya nyumba zao kusombwa na maji.
Katika
Vijiji vya Mbigili na Magole, karibu wakazi wake wote hawana makazi
kutokana na nyumba zao ambazo ni za udongo kujaa maji yaliyofurika
katika Mto Mkundi.
Mkuu wa Wilaya hiyo, Bw. Elias Tarimo ambaye pia
ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa wilayani humo, amekiri mvua hizo kuleta
madhara makubwa kwa wananchi.
Chanzo;Majira
0 comments:
Post a Comment