Home » » Mikoani washangilia mawaziri kung’oka

Mikoani washangilia mawaziri kung’oka

Morogoro
Katika Wilaya za Ulanga na Kilombero mkoani Morogoro, baadhi ya wananchi wameeleza kufurahishwa kwao na uamuzi wa Serikali wa kuwawajibisha mawaziri hao wakisema operesheni hiyo ilisababisha vifo vya watu na wanyama na kwamba hata walipolalamika hawakusikilizwa.
Mmoja wa watu aliyedai kwamba ndugu zake waliuawa katika operesheni hiyo, Hamis Kewala alisema suala la kumalizika kwa ujangili linahitaji umakini kwani wahusika walio wengi wamekuwa wakitumia mbinu mpya kuua tembo na kusafirisha meno hayo, huku wasiohusika wakiumizwa bila hatia.
Mkazi mwingine, Mohamed Nguku alisema: “Vita hii sasa itakosa nguvu, suala la msingi ni kuhakikisha usimamizi wa hali ya juu na umakini, halafu taratibu na sheria za nchi kwa wanaopewa dhamana kufanya kazi hizi lazima zifuatwe na siyo kufanya wanavyojua wao”.
Agosti 12 mwaka huu, Mkazi wa Tarafa ya Mwaya wilayani Ulanga, January Gunena alikamatwa na kupelekwa katika kambi ya mateso iliyokuwa katika Hifadhi ya Selous na  kuteswa na baadaye alifariki dunia.
Wengine waliopatwa na mateso hayo ni madereva wanaoendesha magari yanayofanya safari kati ya Ifakara, Mahenge na Mwaya ambao wakiwa safarini walikuwa wakisimamishwa na askari kuhojiwa lakini wengine wakiishia kupata vipigo na kuporwa fedha.
Chanzo;mwananchi

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa