Morogoro. Mjumbe wa Halmashauri Kuu CCM,
Suleiman Sadiq amewataka viongozi mbalimbali nchini kuhakikisha
wanasimamia vyema miradi inayoanzisha na Serikali ili kutekeleza ilani
ya chama hicho.
Akikagua uhai wa chama na miradi ya maendeleo
katika Kijji cha Manyinga, Kata ya Diongoya, wilayani Mvomero, Sadiq
alisema ni wajibu wa kila kiongozi aliyechaguliwa na CCM kuhakikisha
anatekeleza majukumu yake kikamilifu na kuachana na vijembe au majungu.
Sadiq alisema kufanya hivyo ni kurudisha nyuma jitihada za Serikali kuwaletea wananchi wake maendeleo.
‘’Tunataka kuhakikisha kila kiongozi anawajibika
kwa nafasi yake kuleta maendeleo eneo lake kwa kutekeleza ilani ya
chama, siyo kutupiana lawama mtu anapokosea ni vyema akashauriwa na
kurekebishwa,” alisema Sadiq.
Pia, alisema iwapo viongozi waliochaguliwa au
mwanaCCM yeyote atakwenda kinyume na chama, itasababisha chama kudhofika
na kupoteza majimbo kwa wapinzani.
Sadiq alisema hawawezi kukubali hali hiyo itokee
kwa sababu CCM ni imara na sikivu kwa wananchi wake, hivyo haina budi
kukilinda kwa gharama yoyote ile.
Pia aliwataka viongozi wa mashina na matawi
kuhamashisha wananchi kulipia ada zao za uanachama ili wawe hai sambamba
na kuchangia shughuli au miradi mbalimbali ya kimaendeleo inayoanzishwa
katika maeneo yao ili kuharakisha maendeleo kwani serikali pekee
haiwezi kutekeleza yote.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment