Home » » Majeruhi Mvomero wakimbizwa Muhimbili

Majeruhi Mvomero wakimbizwa Muhimbili



MAJERUHI watatu waliojeruhiwa katika mapambano ya wakulima na wafugaji wilayani Mvomero wamekimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili, jijini Dar es Salaam kwa matibabu zaidi.
Mbali na wagonjwa hao kuhamishiwa Muhimbili katika vitengo mbalimbali kikiwamo cha Mifupa cha Moi, pia watu wengine 14 wameruhusiwa kurejea makwao baada ya hali zao kuendelea vizuri.
Akizungumza na Gazeti hili, Dk. Mashaka Issa, alisema waliohamishiwa katika Hospitali ya Rufaa ni Francis William, Juma Abdi na mwingine ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja.
Awali wakizungumzia hali ya machafuko hayo kwa sasa, Diwani wa kata hiyo, Hembeti Juma Malaja na Ofisa Mtendaji wake, Charles Chikuni alisema imetulia ingawa wananchi bado wana hofu.
Wakati huo huo, Mkuu wa Oparesheni katika Jeshi la Polisi nchini, Paul Chagonja, alisema watu 30 wanashikiliwa na Polisi kuhusiana na mapigano hayo.
Alisema mapigano hayo yalitokana na kukamatwa kwa ng'ombe 300 wa Semwako Matunda wa Mpapa-Hembeti,  waliokuwa wamekula mazao ya watu wanne kijijini hapo. 

Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa