Home » » WANA KIJIJI WAWAJIA JUU VIONGOZI WAO WAPINGA HATUA YA KULAZIMISHWA KUMLIPA MSHAHARA MLINZI WA ZAHANATI YAO

WANA KIJIJI WAWAJIA JUU VIONGOZI WAO WAPINGA HATUA YA KULAZIMISHWA KUMLIPA MSHAHARA MLINZI WA ZAHANATI YAO

 Afisa Mtendaji wa kijiji Cha Melela Bw Fadhiri Mwinyimvua aliyeshjika karatasi akisoma hatua ambayo uongzi wa kijiji hicho unakusudia kuzichukua zidi ya Dr Fulugesi aliyedaiwa kuondoka na vifaa vya Zahanati hiyo  usiku wa mamane na kutafisiliwa kama wizi,wengini ni vigongo wa serikali na Chama cha mapinduzi wa kijiji hicho
 Umati wa wananchi wa kijiji hicho uliokusanyika kwenye ghara cha kuhifadhia chakula baada ya kuchukizwa na hatua ya Daktari huiyo kuondoka na vifaa vya Zahanati yao usiku mnene
 Mmoja wa wananchi wa kijiji hicho akihoji sababu za wagonjwa kutoza  shilingi mia 2 kama gharama za uchagiiaji wa mshahara wa mlini wa Zahanati hiyo
         Zahanati ya kijiji cha Melele
NA DUSTAN SHEKIDELE,MVOMERO.
WANANACHI wa kijiji cha Melela kilichopo wilaya ya Mvomero mkoani hapa,wamepinga hatua ya viongozi wao kuwatoza ushuru wa shilingia 200 wagonjwa wanofika kwenye Zahanati ya kijiji hicho kama gharama za kuchangia mshahara wa mlini za Zanahati hiyo.

Wakizungumza kwa jazba kwenye mkutano uliofanyika juzi kati kwenye ghara la kuhifadhia chakula la kijiji hicho wananchi hao kutibiwa wakidai hatua hiyo kabla ya kutibiwa wamedai jambo hilo ni la uonezi linalowazidishia ukali wa maisha.

" Waheshimiwa tatizo lingine ni hatu ya wagonjwa kutozwa shilingi 200 kwenye Zahanati yetu kabla ya kutibiwa  wananchi kulazimishwa kuchangia mshahara wa Mlinzi tumeliona hapa kwenye Zahanati yetu,naamini pesa zinazopatikana kwa mwezi ni nyingi sana  ingawa siungi mkono wananchi kuradhimishwa kumlipa mlini lakini pia ziada ya fedha hizo zina kwenda wapi na kwa nini sisi wananchi tumlipe mshahara mlini wakati pale hopsital pia tunalipia gharama za matibabu?"alisema mmoja wanakijiji hao

Hivi karibuni wananchi wa kijiji hicho kilichopo wilaya ya Mvomero mkoani hapa waliitisha mkutano kinguvu na kumshutumu daktari mkuu wa Zanahati ya kijiji hicho Dr Fulugesi kuondoka na vifaa vya mamilioni ya shilingi vyakati za usiku.

Mwanakijiji mmoja aliyefahamika kwa jina la Beatus Kanuti ambaye alimsindikiza mgonjwa wake kwenye Zahanati hiyo majira ya saa 5 usiku alishuhudia mtunza stoo wa Zahanati hiyo Bw Mlelwa akitoa vifaa 41 vya upasuaji na kumkabidhi daktari huyo muda huo wa usiku mnene.

Jambo hilo aliluchukulia kama wizi na kuamu kutoa taarifa kwa Afisa mtendaji wa kijiji hicho Bw Fadhiri Mwinyimvua ambaye naye alitoa taarifa kwa kamati ya ulinzi na usalama wa kijiji hicho,ambao kwa pamoja walifika kwenye Zahanati hiyo usiku huo huo na kumkuta daktari huyo ameshatoweka.

Hivyo baada ya kushauriana walimu kwenda nyumbni kwa daktari huyo na baada ya kupekua nyumba yake walifanikiwa kuvikuta vifaa hivyo.ambapo ambapo usiku huo huo wananachi wa kijiji hicho walipeana taarifa na kuamu kuitisha mkutano kujadili jambo hilo.ambapo pia waliamualika Paparazi wa habari hizi kwenye mkutano huo

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa