Home » » News Alert:Mtangazaji Mkongwe hapa nchini julius Nyaisanga afariki Dunia

News Alert:Mtangazaji Mkongwe hapa nchini julius Nyaisanga afariki Dunia


Pichani kati ni Marehemu Julius Nyaisanga akiwa na wadau enzi za uhai wake,pichani kulia ni Othman Michuzi na shoto ni Abhoubakar Lyongo

Mtangazaji mkongwe hapa nchini,aliyekuwa Meneja wa Aboud Media, Julius Nyaisangah,ambaye pia alikuwa mtangazaji wa Radio One na ITV, amefariki dunia leo majira ya saa moja asubuhi katika hospitali ya Mazimbu Mkoani Morogoro.

Taarifa za awali zinasema kuwa marehemu Nyaisanga alikuwa anasumbuliwa na tatizo la shinikizo la damu pamoja na kisukari.

Wakati wa uhai wake, marehemu Nyaisanga aliwahi kufanya kazi sehemu mbali mbali ikiwemo katika makampuni ya IPP ambako alikuwa mkurugenzi wa Radio One pamoja na Radio Tanzania wakati huo ikiitwa RTD ambako alikuwa mtangazaji wa vipindi mbali mbali. Marehemu ameacha mjane na watoto watatu.

Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali pema peponi.
Habari imeandaliwa na Michuzi Blog

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa