Waziri wa
Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba
akipata maelezo kutoka kwa Bw. Mutagabaya Mtaalamu kutoka maabara maalumu ya kutunza Vyura ya
Kihansi.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba akihutubia wananchi wa Kijiji cha Mwantasi Wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa, aliposimama akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua masuala ya mazingira.
Mjumbe wa Kamati ya Mazingira ya Kijiji cha Mwantasi Wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa akipokea kiasi cha Shilingi laki moja zilizotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba kuchangia Mfuko wa Mazingira wa Kijiji.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba na ujumbe wake wakikagua mitambo ya kusukuma maji katika Mkoa wa Iringa, wa kwanza kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bi. Amina Masenza.
*************************************************
Na Lulu
Mussa, Kilolo - Iringa
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa
Rais, Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba amesisitiza umuhimu wa kutunza
Vyanzo vya Maji kwakuwa shughuli zifanywazo na binadamu kando ya Vyanzo hivyo
hupelekea mito hiyo kukauka.
hayo yamebainishwa leo na Waziri
Makamba alipofanya ziara ya kikazi Kihansi Wilayani Kilolo kuangalia chanzo cha
Mto Kihansi. Waziri Makamba kwa nyakati tofauti amefanya mazungumzo na
wanakijiji wa Kijiji cha Mwantasi ambao wamefanya jitihada za dhati kuhifadhi
Vyanzo vya Maji.
Waziri Makamba amewapongea na
kuchangia kiasi cha shilingi laki mbili kwa vijiji vya Mwantasi kwa ajili ya
Mfuko wa Mazingira wa Kijiji wenye lengo la kusimamia masuala za mazingira
katika kijiji chao.
"Nawapongeza sana kwa jitihada mlizonazo
ikiwa ni pamoja na kuwa na sheria ndogo ndogo za kutunza mazingira, nami
nawaunga mkono kwa kuchangia kiasi cha shilingi laki moja kwa kijiji cha
Mwantasi na laki moja kwa kijiji cha Wangama ili kuimarisha mfuko huo"
Makamba alisisitiza.
Aidha Waziri Makamba amemuagiza
Mkurugenzi wa Kilolo kuhakikisha fani zinazotozwa za uharibifu wa mazingira
sehemu ya pesa hizo zinapelekwa katika vijiji husika ili kukuza mfuko huo na
kuwaagiza wajumbe wa Kamati za Mazingira ngazi ya kijiji kuzitunza fedha hizo benki
na kuagiza matumizi sahihi.
Waziri Makamba anaendelea na ziara ya
kikazi katika Mikoa mbalimbali hapa nchini na leo yuko katika Mkoa wa Morogoro
ambapo ametembelea Mto Kihansi na Ruaha Mkuu.
0 comments:
Post a Comment